Sport
Dollar
38,2552
0.34 %Euro
43,8333
0.15 %Gram Gold
4.076,2000
0.31 %Quarter Gold
6.772,5700
0.78 %Silver
39,9100
0.36 %Lissu anashikiliwa katika gereza la Keko kwa tuhuma za Uhaini zinazomkabili.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo nchini Tanzania (CHADEMA) wamelitaka Jeshi la Magereza nchini humo pamoja na vyombo vingine vya dola kueleza alipo Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Tundu Lissu.
Kulingana na taarifa iliyotolewa Aprili 18, 2025 na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA Brenda Rupia, kwa nyakati tofauti, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar Ali Ibrahim Juma, wanachama, mawakili na wanafamilia wamefika katika Gereza la Keko jijini Dar es Salam, ambako anashikiliwa, bila kumuona.
“Hata hivyo, juhudi zao za kumuona Mheshimiwa Lissu hazikufanikiwa baada ya kuelezwa kuwa hayupo katika gereza hilo, cha kusikitisha, hawakupewa maelezo yoyote rasmi juu ya alipopelekwa,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Lissu anashikiliwa katika gereza la Keko kwa tuhuma za Uhaini zinazomkabili.
Comments
No comments Yet
Comment