Dollar

38,4200

0.2 %

Euro

43,6520

-0.28 %

Gram Gold

4.059,5900

-1.7 %

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Tangu Mei 2024 kumekuwa na mapigano makali El-Fasher kati ya jeshi la Sudan na RSF

Jeshi la Sudan lasema limewaua wapiganaji 60 wa RSF Darfur Kaskazini

Siku ya Alhamisi jeshi la Sudan limesema kuwa maafisa wake wamewaua wapiganaji 60 wa RSF mjini El-Fasher, mji mkuu wa jimbo la Darfur Kaskazini magharibi mwa Sudan.

Taarifa kutoka kwa jeshi inasema vikosi vyake pamoja na makundi washirika vilifanikiwa kuwakabili wapiganaji wa RSF magharibi mwa mji huo siku ya Jumatano, na kuwaua 60 pamoja na kuwajeruhi wengine 52.

Kulingana na taarifa hiyo, raia watano waliuawa na wengine 40 kujeruhiwa, ikiwemo wanawake, kutokana na mashambulizi ya RSF katika mji huo siku ya Jumatano.

Kundi hilo la waasi bado halijatoa taarifa yoyote kuhusu tukio hilo.

Kumekuwa na makabiliano makali katika mji wa El-Fasher kati ya jeshi la Sudan na wapiganaji wa RSF tangu Mei 2024, licha ya kuwepo kwa onyo kimataifa kuhusu mapigano katika mji huo, ambao ni sehemu muhimu kwa kuratibu misaada ya majimbo yote matano ya Darfur.

Mapema mwezi huu, RSF ilidai kuchukua udhibiti wa kambi ya wakimbizi ya Zamzam katika mji huo baada ya mapigano na jeshi. Raia wasiopungua 400 waliuawa na watu karibu 400,000 kuondolewa katika makazi hayo kutokana na makabiliano, hii ni kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa.

Tangu Aprili 15, 2023, RSF wamekuwa wakipigana na jeshi la Sudan kutaka kuchukua udhibiti wa nchi, na kusababisha maelfu ya watu kuuawa na kuwepo kwa moja ya hali mbaya kwa watu duniani.

Watu zaidi ya 20,000 wameuawa kufikia sasa, na wengine milioni 15 kuondoka katika makazi yao, kulingana na Umoja wa Mataifa na serikali za mitaa.

Hata Hivyo, Utafiti kutoka kwa wanazuoni wa Marekani, unakadiria kuwa idadi ya waliouawa huenda ikawa 130,000.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#