Dollar

38,1188

0.08 %

Euro

43,4762

0.99 %

Gram Gold

4.014,2000

1.49 %

Quarter Gold

6.511,6500

0 %

Silver

39,6800

0.21 %

Picha mjongeo zilionesha magari ya kivita ya Israeli yakivunja sanamu katika mji wa Yaroun.

Majeshi ya Israeli yavunja sanamu ya Mtakatifu George siku ya Jumapili ya Matawi

Jeshi la Israeli limevunja sanamu ya Mtakatifu George wakati Wakristu wa kusini mwa Lebanoni wakiwa wanasheherekea Jumapili ya Matawi.

Kulingana na chombo cha habari cha taifa la Lebanon (NNA), sanamu hiyo iliharibiwa siku ya Jumapili katika mji wa mpakani wa Yaroun.

"Picha mjongeo zimeonesha magari ya kivita yakivunja sanamu hiyo,” kilisema chombo cha habari cha Lebanon.

Waziri wa kazi wa zamani wa Lebanon Moustafa Bayram, aliweka picha hiyo kwenye ukurasa wake wa X.

“Bila aibu, jeshi la Israeli lilirekodi tukio hili, likionesha kusudio lao la kuendeleza udhalimu wao," alisema.

Hata hivyo, hapakuwa na tamko lolote kutoka kwa jeshi la Israeli kuhusiana na tukio hilo.

Wakristu wote ulimwenguni huadhimisha siku ya Jumapili ya Matawi kama kumbukumbu ya Yesu Kristo kuingia Yerusalemu, akijiandaa na mateso yake, kifo chake na kufufuka kwake, kulingana na imani ya Kikristo.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#