Sport
Dollar
38,4196
0.2 %Euro
43,6867
-0.2 %Gram Gold
4.069,8100
-1.45 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy amesema amelazimika kukatisha sehemu ya ratiba yake nchini Afrika Kusini baada ya shambulizi la Urusi katika mji mkuu wa Kyiv.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy atakatisha ziara yake nchini Afrika Kusini baada ya mashambulizi ya Urusi katika mji mkuu wa Kyiv kuwaua takriban watu tisa.
Rais Zelenskyy aliwasili Afrika Kusini Alhamisi asubuhi kwa mazungumzo na Rais Cyril Ramaphosa wa nchi hiyo kuhusu ushirikiano wa pande mbili na juhudi za kumaliza vita vya Urusi nchini Ukraine.
“Ninakatisha sehemu ya ratiba ya ziara hii na nitarejea Ukraine mara tu baada ya mkutano na Rais wa Afrika Kusini,” alisema katika mtandao wa jamii.
“Leo, nitamueleza Rais Ramaphosa wa Afrika Kusini, ambaye kwa sasa anashikilia Urais wa G20, kuhusu hali na haja yetu ya kuimarisha juhudi za kidiplomasia duniani. Mashambulizi lazima yakomeshwe mara moja na bila masharti,” aliongezea.
“Pia tunategemea uungwaji mkono katika masuala ya kibinadamu - katika kuwarudisha wafungwa wetu na watoto wa Kiukreni waliotekwa nyara na Urusi,” Rais Zelenskyy aliongezea.
Rais Zelenskyy amesema shughuli za uokoaji zinaendelea, na vifusi vya majengo ya makazi vinaondolewa. Kufikia Alhamisi asubuhi amesema zaidi ya watu 80 wamejeruhiwa kote Ukraine huku 9 wakiuawa.
Comments
No comments Yet
Comment